MARUFUKU KWA WAGOMBEA WA URAIS KUFANYA KAMPENI KWENYE MIKUSANYIKO ISIYO RASMI – NEC

MARUFUKU KWA WAGOMBEA WA URAIS KUFANYA KAMPENI KWENYE MIKUSANYIKO ISIYO RASMI – NEC

Like
179
0
Wednesday, 26 August 2015
Local News

TUME ya Taifa ya Uchaguzi imevitaka vyama vya siasa kuzingatia ratiba ya kampeni ya uchaguzi wa rais kwa kufanya mikutano kwa tarehe, sehemu na mahala kwa mujibu wa ratiba.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na NEC, vyama vyote vya siasa vinatakiwa vizingatie ratiba ya kampeni ya uchaguzi wa rais na viache kufanya mikusanyiko ya aina yoyote ambayo haipo katika ratiba ya kampeni hizo.

Chama kitakachokiuka maelekezo hayo kitakuwa kimekiuka kipengele cha maadili ambacho kinaelekeza kuwa ni wajibu wa vyama vya siasa na wagombea kuheshimu na kutekeleza sheria za uchaguzi, kanuni za uchaguzi, maadili ya uchaguzi na maelekezo ya tume ya taifa ya uchaguzi pamoja na sheria zingine za nchi katika kipindi chote cha uchaguzi.

Comments are closed.