MATEKA 70 WAKOMBOLEWA KWENYE MIKONO YA IS

MATEKA 70 WAKOMBOLEWA KWENYE MIKONO YA IS

Like
179
0
Friday, 23 October 2015
Global News

WANAJESHI wa Marekani wakishirikiana na wanajeshi wa Iraq wamefanikiwa kuwakomboa mateka 70 waliokuwa wakizuiliwa na wapiganaji wa Islamic State (IS) nchini Iraq.

Idara ya ulinzi ya Marekani imesema operesheni ya kuwakomboa mateka hao ilitekelezwa baada ya kubainika kwamba walikuwa karibu kuuawa.

Lakini mwanajeshi wa Marekani aliyejeruhiwa kwenye operesheni hiyo amefariki na ndiye mwanajeshi wa kwanza kufariki tangu kuanza kwa operesheni ya wanajeshi wa Marekani dhidi ya IS mwaka jana.

 

 

Comments are closed.