MERCELL JENSEN ATANGAZA KUSTAAFU SOKA

MERCELL JENSEN ATANGAZA KUSTAAFU SOKA

Like
158
0
Thursday, 09 July 2015
Slider

Mlinzi wa zamani wa Ujerumani Marcell Jansen ametangaza maamuzi ya kustaafu soka akiwa na miaka 29 na kusema hana mpango wa kutafuta klabu nyingine baada ya kumaliza kuitukikia Hamburg SV.

Beki huyo wa kushoto ambae pia ameichezea Moenchengladbach na Bayern Munich kabla ya kukipiga kwa miaka saba kwenye klabu ya Hamburg. Amesema amepokea ofa kutoka klabu mbalimbali ila angependelea kuingia kwenye fani nyingine mbali na kucheza mpira. Aliandika kupitia ukurasa wake wa facebook.

Jansen aliyecheza kombe la dunia mwaka 2006 na 2010 ameongez kuwa ameridhishwa na mafanikio aliyoyapata kupitia mchezo wa soka hivyo ni muda wake sasa kufanya mambo mengine tofauti na mpira

Comments are closed.