MGONJWA WA EBOLA ABAINIKA HISPANIA

MGONJWA WA EBOLA ABAINIKA HISPANIA

Like
301
0
Tuesday, 07 October 2014
Global News

Uchunguzi unaendelea katika hospitali ya Madrid nchini Hispania kutokana na muuguzi mmoja nchini humo kuwa mtu wa kwanza kubainika kuwa na virusi vya ugonjwa wa Ebola anaodaiwa kuwa aliambukizwa virusi vya ugonjwa huo kutoka nchi za Afrika Magharibi.

EBOLA MADRID

Muuguzi huyo alikuwa miongoni mwa kikosi cha madaktari waliowatibia raia wamisionari wawili waliokufa kutokana na ugonjwa huo baada ya kurejeshwa nyumbani kwao wakitokea nchi za Afrika Magharibi.

Hata hivyo hospitali hapo kwa sasa kuna uangalizi mkubwa huku vifaa vya kujikinga na vifaa vya kiafya ili kuzuia maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo.

zaidi ya watu 3000 kutoka Afrika Magharibi wamekufa kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mlipuko wa ugonjwa huo uliotokea hivi karibuni.

 

Comments are closed.