MJADALA WA USALAMA WA NYUKLIA KUFANYIKA WASHINGTON

MJADALA WA USALAMA WA NYUKLIA KUFANYIKA WASHINGTON

Like
202
0
Friday, 01 April 2016
Global News

VIONGOZI zaidi ya 50 wa mataifa na serikali pamoja na wawakilishi wa mashirika kadhaa ya kimataifa wanakutana mjini Washington kuzungumzia usalama wa nyuklia.

Hofu ya kutokea mashambulio ya kigaidi kutokana na kuibiwa vifaa vya nyuklia na kutapakaa silaha hizo ndio chanzo cha mkutano huo wa kilele ulioitishwa na Rais Barack Obama wa Marekani.

Pia kitisho cha nguvu za nyuklia za Korea Kaskazini ni miongoni mwa mada kwenye mazungumzo hayo.

Comments are closed.