MAKUNDI NA RATIBA KUELEKEA MICHUANO YA ATP WORLD TOURS LONDON

MAKUNDI NA RATIBA KUELEKEA MICHUANO YA ATP WORLD TOURS LONDON

Like
325
0
Tuesday, 04 November 2014
Slider

TENNIS

Kuelekea katika michuano ya ATP World Tours pale jijini London nchini England, makundi na ratiba ya michuano hiyo inayotarajiwa kuanza tarehe 9 mpaka 16 mwezi huu yapangwa rasmi hapo jana usiku.

Bingwa namba moja katika mchezo huo, Novak Djokovic amepangwa katika kundi A pamoja na wachezaji wengine watatu nafasi zao duniani katika mabano, Satnislas Wawrinka (4), Tomas Berdych (7) na Marin Cilic (9).

Katika kundi B limewakutanisha vigogo Roger Federer anayesika nafasi ya pili kwa ubora duniani, Muingereza Andy Murray huku Kei Nishikori (5) na Milos Raonic (8) wakikamilisha washiriki wa kundi hilo.

Wachezaji wawili watakaomaliza nafasi mbili za juu katika makundi hayo watatinga moja kwa moja kwenye hatua ya nusu fainali huku Djokovic na Federer wakiwa wanachuana kumaliza mwaka kama bingwa namba moja.

Comments are closed.