MOURINHO: KUTETEA TAJI NI KAZI NGUMU

MOURINHO: KUTETEA TAJI NI KAZI NGUMU

Like
176
0
Thursday, 06 August 2015
Slider

Meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho anahisi itakuwa vigumu zaidi kwa upande wake kutetea taji la ligi kwa wapinzani licha ya klabu hizo kuwa zimefanya usajili mzuri na imara kwa vikosi vyao.

Chelsea ilitwaa taji katika msimu uliopita, ikimaliza na alama 87, ikiwa na alama nane mbele ya Manchester City.

“mwaka uliopita tuliwachukua Costa na Fabregas  ikiwa ni maamuzi ya haraka licha ya kuwa hatukufanikiwa kutwaa taji” alisema Mourinho told katika mahojiano yake na kituo cha Sky Sports.

“mwaka huu unaweza kuona hali za Liverpool, Arsenal Man City, Man United wamejiweka imara zaidi kwakufanya usajili imara kwenye vikosi vyao ili kutwaa taji la ligi ila hawatopata taji hilo.

Mourinho anatajia kufunga mbio za ligi kuu huku timu yake ikiwa na alama chache zaidi pia zikiwemo timu ndogo na kuwavutia wachezaji imara katika ligi.

“huenda mawazo yangu yakawa sio sahihi lakini wazo la kumaliza msimu wa ligi na alama chache itatupa ushindi” aliongeza mreno huyu mwenye miaka 52.

“timu ndogo zimefanya usajili kwakutazama wachezaji wazuri kutoka mataifa mbalimbali wenye nia zaidi ya kutaka kuonyesha vipaji vyao

Comments are closed.