MTWARA KWAZUKA GONJWA LA AJABU

MTWARA KWAZUKA GONJWA LA AJABU

Like
473
0
Tuesday, 18 November 2014
Local News

JUMLA ya Wanafunzi wa Kike 45 na Mwalimu Mmoja wamekubwa na ugonjwa wa ajabu ambao haujapata dawa hadi sasa kwenye Kata ya Chingungwe Wilaya ya Tandahimba Mkoa wa Mtwara.

Baraza la Madiwani la Wilaya ya Tandahimba limeelezwa kuwa ugonjwa huo unawakumba watoto wa Kike tu ambapo huanguka na kupoteza fahamu pindi waingiapo maeneo ya shule ya Sekondari ya Chingungwe.

Akito taarifa ya utekelezaji wa Mradi ya Kata ya Chingungwe kwenye Baraza la Madiwani Diwani HALIMA MCHUNGA amebainisha kuwa watoto hao wa Kike hukumbwa na ugonjwa huo mara tu waingiapo eneo la Shule lakini siyo wanapokuwa nje ya eneo la Shule.

 

Comments are closed.