MYANMAR: KIONGOZI WA UPINZANI ATOA WITO KUFANYIKA MAZUNGUMZO YA KITAIFA

MYANMAR: KIONGOZI WA UPINZANI ATOA WITO KUFANYIKA MAZUNGUMZO YA KITAIFA

Like
131
0
Wednesday, 11 November 2015
Global News

KIONGOZI wa upinzani nchini Myanmar Aung Suu Kyi, leo ametoa  wito  wa kuwepo kwa  mazungumzo  ya  kitaifa  ya upatanishi  kati ya rais  wa  Myanmar  na  mkuu  wa  jeshi  la nchi  hiyo  lenye  nguvu  kubwa  kisiasa  baada ya chama chake kuonekana  kupata  ushindi  wa  kishindo katika Uchaguzi mkuu.

Chama  cha  National League for  Demcracy-NLD-kimeonekana kupata madaraka  baada  ya  kupata asilimia  90  ya  viti vilivyotangazwa  hadi  sasa sawa na viti 163 kati  ya  viti 182 vilivyotangazwa  hadi sasa.

Licha  ya maafisa  wa  uchaguzi  kutotangaza kwamba  chama  cha  NLD  kimeshinda, madaraka  ya nchi  hiyo  yaliyokuwa  mikononi  mwa  jeshi  kwa  nusu karne , yanaelekea kubadilika.

Comments are closed.