MZOZO WA SYRIA: MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE ULAYA KUKUTANA LEO

MZOZO WA SYRIA: MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE ULAYA KUKUTANA LEO

Like
157
0
Monday, 12 October 2015
Global News

MAWAZIRI wa Mambo ya nje wa nchi za Umoja wa Ulaya wanakutana leo Luxembourg kujadili njia za kuutafutia ufumbuzi mzozo nchini Syria.

Mkutano huo unafanyika huku kukiwa na wasiwasi kuhusu hatua ya Urusi kujiingiza kijeshi katika mzozo huo na mustakabali wa rais wa Syria Bashar al Assad ukiwa haujulikani.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, mzozo wa Syria umesababisha watu wapatao 250,000 kuuawa tangu mwaka 2011.

Comments are closed.