NATO YAIUNGA MKONO UTURUKI KUTUNGUA NDEGE YA URUSI

NATO YAIUNGA MKONO UTURUKI KUTUNGUA NDEGE YA URUSI

Like
200
0
Wednesday, 25 November 2015
Global News

 JUMUIA ya kujihami ya nchi za magharibi NATO imesema inasimama pamoja na Uturuki baada ya kuitungua ndege ya kivita ya Urusi.

 

Akizungumza baada ya mkutano wa dharura ulioitishwa na Uturuki, Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema tathmini ya tukio hilo inaonyesha kuwa ndege ya kivita ya Urusi iliruka katika anga ya Uturuki.

 

Huku kukiwa na hali ya wasiwasi, Stoltenberge ametaka kuwepo na hali ya utulivu kutoka pande zote.

Comments are closed.