NEW YORK CITY: FRANK LAMPARD AFURAHIA KUKIPIGA NA LAMPARD PAMOJA NA PIRLO

NEW YORK CITY: FRANK LAMPARD AFURAHIA KUKIPIGA NA LAMPARD PAMOJA NA PIRLO

Like
162
0
Wednesday, 08 July 2015
Slider

Kiungo wa zamani wa England Frank Lampard amesema anajisikia faraja na mwenye bahati kukipiga katika timu moja ya New York City  na Andrea Pirlo

Mchezaji huyo wa zamani wa klabu za  Chelsea na Manchester City,37 aliwekwa wazi na klabu ya New York siku ya jumanne akiwa tayari kukipiga katika mchezo wake wa kwanza na klabu hiyo dhidi ya Toronto tarehe 12 July.

Klabu hiyo ya New York pia amemuongeza muitalia Andrea Pirlo, 36, kutoka Juventus kuongeza nguvu kwenye kikosi pamoja na David Villa.

“David na Andrea wapo kwenye orodha ya juu, najiona mwenye bahati kuwa kwenye kikosi kimoja” alisema Lampard.

“nimekuwa nikifuatilia michezo yote. Namjua kila mchezaji na jinsi wanavyocheza hivyo ni jambo la faraja kucheza nao kila siku” aliongeza Lampard

 

Comments are closed.