PAKISTAN: WALIOPANGA NDOA YA WATOTO WAKAMATWA

PAKISTAN: WALIOPANGA NDOA YA WATOTO WAKAMATWA

Like
223
0
Friday, 04 March 2016
Global News

POLISI waliopo Mashariki mwa Pakistan wamewakamata watu wanne wanaotuhumiwa kupanga ndoa kati ya mvulana mwenye umri wa miaka 14 na msichana mwenye umri wa miaka 10 pekee suala ambalo ni kinyume cha sheria.

Imeelezwa kwamba ndoa hiyo ilikuwa imepangwa kama njia ya kusuluhisha mzozo baina ya familia hizo mbili.

Tabia ya kuendeleza ndoa za mapema pamoja na kutatua mizozo ya nyumbani kupitia ndoa, ni hatia kwa mujibu wa sheria za Pakistan.

Comments are closed.