POPCAAN KUSHIRIKI KWENYE COLLABO NA YOUNG THUG

POPCAAN KUSHIRIKI KWENYE COLLABO NA YOUNG THUG

Like
229
0
Friday, 29 May 2015
Entertanment

Star wa muziki wa Dancehall Popcaan amepata nafasi ya kushiriki kwenye wimbo wa I Know There’s Gonna Be (Good Times) katika project inayoaandaliwa na producer wa Uingereza Jamie xx, wimbo huo pia utamhusisha rapa Young Thug. kutokea Marekani.

Hii si mara ya kwanza kwa msanii huyu kushiriki kwenye collabo za kimataifa kwani aliwahi pia kushirikiana na msanii wa Uingereza Melissa Steele kwenye ngoma ya single Kisses for Breakfast.Iliyofanya vizuri kwenye UK Top 10 chart.

Mbali na hiyo pia sauti yake iliwahi kutumika kama sample kwenye ngoma ya Kanye west Guilt Trip inayopatikana kwenye albam ya Yeezus ya mwaka 2013.

Jamie xx ni producer mkubwa duniani kwani amewahi kuproduce kazi za wasanii kama Alicia Keys, Drake pia amefanya  ngoma iliyobeba jina la albam ya Drake Take Care ambayo ni colabo na rihana iliyotoka mwakan 2011 hivyo ni nafasi nzuri kwa Popcaan pia kuzidi kuutangaza muziki wake.

 

Comments are closed.