RAIS KIKWETE AKUBALI KUJIUNGA NA KUNDI LA WATU MASHUHURI DUNIANI KWENYE MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA

RAIS KIKWETE AKUBALI KUJIUNGA NA KUNDI LA WATU MASHUHURI DUNIANI KWENYE MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA

Like
247
0
Wednesday, 30 September 2015
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta Jakaya Mrisho Kikwete ameombwa na amekubali kujiunga na kundi la watu mashuhuri duniani wakiwemo viongozi wa Afrika, matajiri wa Marekani na watu wengine mashuhuri katika kutafuta majawabu ya kumaliza ugonjwa wa malaria duniani kwa kuanzia na Bara la Afrika.

 

Ombi hilo kwa Rais Kikwete kujiunga na kundi hilo ambalo litaongozwa na tajiri mkubwa zaidi duniani, Bwana Bill Gates, liliwasilishwa kwa mara ya kwanza kwake wiki iliyopita na Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa wa Kupambana na Malaria, Bwana Ray Chambers, tajiri mwingine wa Marekani

Comments are closed.