RAIS KIKWETE,DK.SHEIN WAWASILI MJINI DODOMA

RAIS KIKWETE,DK.SHEIN WAWASILI MJINI DODOMA

Like
647
0
Wednesday, 08 October 2014
Local News

 

 

KIKWETE

Rais wa jamuhuli ya muungano wa Tanzania Mh Jakaya mrisho Kikwete amewasili mjini Dodoma leo katika Hafla maalum ya kukabiziwa katiba iliyopendekezwa na bunge maalum la katiba

mheshimiwa Rais amepokelewa katika uwanja wa Jamuhuli mjini Dodoma.

SHAIN

Rais wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na aliyekua Spika wa Bunge la Malum la Katiba Samuel Sitta alipowasili Uwanja wa Ndege wa Dodoma leo kuhudhuria katika Hafla ya kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na Bunge Maalum la katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma.

Tukio hilo la kihistoria linahitimisha mchakato wa kikao cha Bunge maalum la Katiba kilichomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita kwa kuipitisha katiba tarajiwa kwa zaidi ya theluthi mbili ambapo kwa sasa inasubiri kupelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni hapo mwakani.

Huku katiba hiyo mpya iliyopendekezwa ikitarajiwa kuwasilishwa kwa rais baadaye hii leo, suala la kutojumuishwa moja kwa moja kwa mahakama ya kadhi katika katiba hiyo linaendelea kuwakera baadhi pamoja na serikali kuahidi kuliwasilisha bungeni kwa majadiliano zaidi hapo baadaye.

 

Comments are closed.