RAIS WA KRIKETI INDIA AFARIKI DUNIA

RAIS WA KRIKETI INDIA AFARIKI DUNIA

Like
240
0
Monday, 21 September 2015
Slider

Rais wa bodi ya Kriket ya India Jagmohan Dalmiya amefariki dunia. Dalmiya mwenye miaka 75 alifikishwa hospitalini siku ya Alhamisi wiki iliyopita kutokana na maumivu ya kifua huku akilazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Amehudumu katika nafasi ya Urais wa Kriket nchini humo tokea mwaka 2001 mpaka 2004 kwa kipindi cha mpito wa uongozi wa chama hicho ambapo alirudi tena madaraani mwaka 2013 mpaka Machi 2015.

Alikuwa pia kiongozi katika shirikisho la dunia la mchezo huotokea mwaka 1997 mpaka 2000.

Comments are closed.