RAIS WA UJERUMANI AWASILI NCHINI

RAIS WA UJERUMANI AWASILI NCHINI

Like
212
0
Tuesday, 03 February 2015
Local News

RAIS wa Ujerumani JOACHIM GAUCK na msafara wake amewasili nchini .

Mara baada ya kuwasili akiwa ameambatana na mkewe Bibi SCHADT  amelakiwa na Makamu wa Rais Dokta  MOHAMED GHARIB BILALI pamoja  na burudani za ngoma za asili kutoka vikundi mbalimbali na wananchi waliojitokeza kumpokea.

Rais huyo  ambaye anaitembelea Tanzania kwa mara ya kwanza kufuatia  mwaliko kutoka kwa Rais JAKAYA KIKWETE leo amepokelewa katika viwanja vya Ikulu majira ya saa 3 asubuhi ambapo Rais huyo akiwa na mwenyeji wake, JAKAYA KIKWETE atapata fursa ya kukagua gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili yake na Jeshi la Wananchi wa Tanzania na kupigiwa mizinga 21.

G2 G3

 

Comments are closed.