RONALDO AONYESHA NIA YA KUBAKI REAL MADRID

RONALDO AONYESHA NIA YA KUBAKI REAL MADRID

Like
165
0
Tuesday, 09 February 2016
Slider

Nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amesema hataki kuondoka klabuni hapo kabla ya mkataba wake kumalizika mwaka 2018.

Mreno huyo mwenye miaka 31 amekua akihusishwa na kurudi kujiunga na timu yake ya zamani ya Manchester United, ambayo ilimuuza mwaka 2008 au Paris St-Germain, ya Ufaransa.

“Nataka kubakia hapa kwa miaka miwili zaidi, miaka miwili ninayozungumzia itanichukua mpaka mwisho wa maktaba wangu, “alinukuliwa mchezaji huyo.

Ronaldo alizungumza hayo wakati ya ghafla ya uchukuaji tuzo ya Pichichi, amabpo alishinda tuzo hiyo baada ya kuwa mfungaji bora mismu uliopita kwa kufunga mabao 48.

“Hii ni ligi bora duniani, japo kuwa pia nimecheza ligi ya England, ni ligi ya ushindani na inawachezaji wazuri.”

Comments are closed.