SERIKALI KUPAMBANA NA WAFANYABIASHARA WAKUBWA WA DAWA ZA KULEVYA

SERIKALI KUPAMBANA NA WAFANYABIASHARA WAKUBWA WA DAWA ZA KULEVYA

Like
204
0
Thursday, 06 November 2014
Local News

SERIKALI kupitia Tume ya kudhibiti dawa za kulevya inaandaa mikakati ya kupambana na wafanyabiashara wakubwa wa dawa  hizo ili kunusuru makundi ya vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa.

Hayo yamebainishwa na Afisa Tawala Tume ya kudhibiti dawa za kulevya AIDA TESHA alipotembelea kituo cha kutibu waathirika wa dawa hizo cha PILI FOUNDATION kilichopo Kigamboni jijini Dar es salaam.

TESHA ameeleza kuwa ili kudhibiti matumizi ya dawa hizo ni vyema kupambana na wafanyabiashara wakubwa badala ya kushughulika na wafanyabiashara wadogo.

Comments are closed.