TANZANIA INAUNGA MKONO KWA DHATI UMOJA WA AFRIKA NA USHIRIKIANO WA EAC

TANZANIA INAUNGA MKONO KWA DHATI UMOJA WA AFRIKA NA USHIRIKIANO WA EAC

Like
291
0
Monday, 23 February 2015
Local News

Tanzania inaunga  mkono kwa dhati Ushirikiano  wa Kikanda na muumini mkubwa wa Umoja wa Africa na Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki -EAC.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo jijini Nairobi mara baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa EAC na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ambaye amekua mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita

Rais  Kikwete amesema na kumpongeza Rais Kenyatta kwa kusimamia utekelezwaji wa maazimio na miradi ya pamoja ya Jumuiya wakati wa kipindi chake cha uenyekiti na kuahidi kuwa Tanzania haitawaangusha wana Afrika Mashariki katika kutekeleza azma yao ya pamoja ya kuendeleza Jumuiya ambayo inaundwa na nchi za Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.

EAC EAC3 EAC4 EAC5 EAC6 EACCC

Comments are closed.