TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA WAHASIBU KIMATAIFA

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA WAHASIBU KIMATAIFA

Like
269
0
Thursday, 05 February 2015
Local News

Tanzania itakuwa mwenyeji wa mkutano wa 22 wa kimataifa wa Chama cha Wahasibu Wakuu wa Serikali wa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika –ESAAG, utakaofanyika nchini kuanzia Machi 09, hadi 12 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa na Mhasibu Mkuu wa Serikali Mwanaidi Mtanda kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dokta. Servacius Likwelile jijini Dar es salaam alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano huo utakaofanyika nchini.

Amesema kuwa mgeni rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Kikwete.

MTANDA2

Comments are closed.