Tiangong-1: Kituo cha safari za anga cha Uchina kinaweza kuanguka duniani ”karibuni”

Tiangong-1: Kituo cha safari za anga cha Uchina kinaweza kuanguka duniani ”karibuni”

Like
378
0
Tuesday, 27 March 2018
Global News

Kifusi kutoka kwa kituo cha maabara cha safari za anga cha China, kinaweza kupasuka na kuanguka duniani Ijumaa,wanasayansi wanaokifanyia uchunguzi wanasema.
Kituo hicho cha Tiangong-1 ni sehemu ya mpango wa safari za anga za mbali wa Uchina, na wa sampuli ya kituo cha safari za anga za mbali cha binadamu wa mwaka 2022.
Kiliwekwa kwenye uzio mwaka 2011 na miaka mitano baadae kikamilisha shughuli yake, na baadae kilitarajiwa kuanguka duniani.
Muda na mahala kitakapoangukia ni vigumu kutabiri kwasababu sasa hakidhibitiwi.
Makadirio ya hivi karibuni ya kurejea kwa chombo hicho ni kati ya tarehe 30 Machi na 2 Aprili.

Comments are closed.