TOYOTA YAAGIZA MAGARI MILIONI MOJA YARUDISHWE KIWANDANI

TOYOTA YAAGIZA MAGARI MILIONI MOJA YARUDISHWE KIWANDANI

Like
541
0
Wednesday, 15 October 2014
Global News

toy_showroom_lg

Kampuni kubwa zaidi ya kuunda magari, Toyota, imeagiza kurejeshwa kwa magari milioni moja nukta saba kote duniani kutokana na hitilafu ya breki za magari hayo.

Kampuni hiyo imesema hitilafu tatu zimetambulika kwenye breki katika miundo mbali mbali za magari ya Toyota ikiwemo muundo wa Lexus.

Magari yaliyo ndani na nje ya Japan yote yameathiriwa na hitilafu hizo.

Hata hivyo kampuni yenyewe imesema haina habari yoyote kuhusu ajali za magari au watu kujeruhiwa kutokana na hitilafu hizo.

Wadadisi wanasema hili ni jambo la kuaibisha sana kwa Toyota ambayo imelazimika kuagiza magari yake kurejeshwa kiwandani zaidi ya mara moja kutokana na hitilafu mbali mbali.

 

Comments are closed.