UCHIMBAJI WA KOKOTO MARUFUKU TEMEKE

UCHIMBAJI WA KOKOTO MARUFUKU TEMEKE

Like
378
0
Friday, 22 January 2016
Local News

MKUU wa Wilaya ya Temeke Sofia Mjema amepiga marufuku shughuli za uchimbaji Kokoto na Mchanga zinazofanyika kigamboni pamoja na maeneo mengine ya Manispaa ya Temeke kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira unaofanyika  kupitia shughuli hizo.

 

Mjema amechukua maamuzi hayo baada ya kutembelea maaneo hayo akiambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Manispaa ya Temeke ambapo amebaini uharibifu mkubwa wa mazingira unaofanyika kupitia shughuli hiyo huku akirejea Kauli ya Mkuu wa Mkoa Dar es salaam Said Meck Sadick kua Dar es salaam haina maeneo yalioandaliwa kwa ajili ya uchimbaji mchanga na kokoto.

Comments are closed.