UMOJA WA NCHI ZA MAGHARIBI WATAKA HATUA KALI ZICHUKULIWE MZOZO WA UKRAINE

UMOJA WA NCHI ZA MAGHARIBI WATAKA HATUA KALI ZICHUKULIWE MZOZO WA UKRAINE

Like
168
0
Wednesday, 04 March 2015
Global News

VIONGOZI wa nchi za Magharibi wamekubaliana kwamba hatua kali kutoka kwa Jumuiya ya Kimataifa zitahitajika iwapo kutatokea ukiukaji wa utekelezaji wa Mkataba wa kusitisha mapigano nchini Ukraine.

Mkataba huo umesainiwa Mjini Minsk nchini Belarus Febrauari 12 mwaka huu kati ya majeshi ya Serikali ya Ukraine na Waasi wanaoiunga mkono Urusi.

Rais wa Marekani BARACK OBAMA, mwenzake wa Ufaransa FRANCOIS HOLLANDE, Kansela wa Ujerumani ANGELA MERKEL, Waziri Mkuu wa Uingereza DAVID CAMERON na Waziri Mkuu wa Italia MATTEO RENZI wameshiriki katika mkutano kwa njia ya video kuhusu mzozo wa Ukraine.

Comments are closed.