VODACOM YATANGAZA KUMPATA MSHINDI WA APPSTAR

VODACOM YATANGAZA KUMPATA MSHINDI WA APPSTAR

Like
233
0
Wednesday, 17 December 2014
Local News

KAMPUNI ya simu za Mkononi ya Vodacom, imetangaza kumpata mshindi bora wa ubunifu wa program za simu kupitia shindano la AppStar linaloendeshwa na Kampuni hiyo.

Kwa Mujibu wa Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Abigail Ambweni, kupitia program hiyo Mshindi wa kwanza atakwenda India kushiriki katika ngazi ya kimataifa.

 Mshindi kuyo ni Roman Mbwasi ambaye ameibuka kidedea katika shindano la kutafuta vipaji vya ugunduzi wa program za simu la AppyStar lililoandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania likiwa linawalenga  wanafunzi wa vyuo vikuu wanaosoma  masomo ya Sayansi ya Teknolojia ya habari na Mawasiliano na watanzania wote.

 

Comments are closed.