WAANDAMANAJI WAFANYA VURUGU UTURUKI

WAANDAMANAJI WAFANYA VURUGU UTURUKI

Like
211
0
Wednesday, 09 September 2015
Global News

MAELFU  ya waandamanaji waliokuwa wakipeperusha bendera za Uturuki wamevamia makao makuu ya chama kikuu cha Kikurdi cha HDP.

Jengo hilo lililoko katika mji mkuu wa Ankara baada ya kuvamiwa lilichomwa moto.

Waziri mkuu wa Uturuki Ahmet Davutoglu amelaani vikali mashambulizi na uvamizi huo katika ofisi za kisiasa na hata kwa nyumba za habari na ametoa wito wa kusitisha ghasia.

Comments are closed.