WAASI WA ADF WASHAMBULIA DRC

WAASI WA ADF WASHAMBULIA DRC

Like
413
0
Thursday, 16 October 2014
Global News

Jeshi la DRC linasema kuwa watu 26 wameuawa nchini humo katika shambulizi liliofanywa katika mji wa Beni Mashariki mwa nchi.

Wengi, wa waliofariki walikuwa raia wakiwemo watoto.

Shirika moja la kutetea haki za binadamu, linasema kuwa wapiganaji wa kundi la waasi la Uganda la ADF au Allied Democratic Forces , lilivamia mji huo nyakati za usiku.

Kikosi cha Umoja wa Matifa kikishirikiana na wanjeshi wa DRC, kimekuwa kikijaribu kuwatimua waasi hao wa ADF kutoka nchini DRC tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

Lakini waasi hao nao pia wamekuwa wakifanya mashambulizi kadhaa katika meizi ya hivi karibuni.

 

Comments are closed.