WANAFUNZI WAFANYA MAANDAMANO KUPINGA MKUTANO WA CHINA NA TAIWAN

WANAFUNZI WAFANYA MAANDAMANO KUPINGA MKUTANO WA CHINA NA TAIWAN

Like
244
0
Wednesday, 04 November 2015
Global News

MAELFU ya wakazi na wanafunzi wameandamana leo nje ya jengo la Bunge la Taiwan, kutokana na kughadhibishwa na mkutano wa kihistoria ulipangwa kufanywa na viongozi wa Taiwan na China.

 

Rais wa Taiwan  Ma Ying-jeou anatarajiwa kukutana na rais wa China  Xi Jinping  Jumamosi mjini Singapore.

 

Mashirika ya habari ya umma yameripoti kwamba, mkutano huo utakuwa wa kwanza kwa viongozi wa China na Taiwan kukutana katika kipindi cha miongo sita.

Comments are closed.