WANAWAKE 100 WA JAMII YA KIMASAI WAANDAMANA NA KULALA MSITUNI

WANAWAKE 100 WA JAMII YA KIMASAI WAANDAMANA NA KULALA MSITUNI

Like
315
0
Tuesday, 25 November 2014
Local News

 

ZAIDI ya Wanawake 100 wa Jamii ya Kimasai wameandamana na kwenda kulala msituni kwa muda wa siku mbili wakipinga kitendo cha Serikali kukata miti ya Asili katika kijiji cha Matebete ,Kata ya Itamboleo Wilaya ya Mbarari mkoani Mbeya.

Wanawake hao wamechukua uamuzi huo wakipinga hekta zaidi ya 30,000 za miti wanayoitegemea katika shughuli zao kukatwa bila wao kushirikishwa.

Mmoja wa Wanawake hao aliefahamika kwa jina la SOFIA KALEI ameeleza kuwa hawako tayari kuona msitu huo ukiteketezwa kwa sababu umekuwa ukiwasaidia katika shughuli mbalimbali.

Comments are closed.