WATANZANIA WAMETAKIWA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA

WATANZANIA WAMETAKIWA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA

Like
156
0
Wednesday, 29 July 2015
Local News

WATANZANIA wametakiwa kujiepusha na vitendo vya rushwa kwani vitawafikisha pabaya na kurudisha maendeleo yao nyuma hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi  mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini-Takukuru, Dokta Edward Hosea katika mafunzo ya maafisa wa Taasisi hiyo juu ya  utakatishaji fedha na kupata taarifa na mlolongo wa uhalifu kwa kutumia sheria za Tanzania.

Dokta Hosea amesema mafunzo hayo yatawasaidia maafisa hao kupata na kuelewa vithibitisho vya uhalifu vinavyogusa fedha na mali zilizopatikana kwa rushwa na kutaifisha mali chini ya sheria ya Tanzania ya utakatishaji wa fedha ya mwaka 2006.

 

Comments are closed.