WAZIRI MKUU WA UFARANSA ATOA TAHADHALI DHIDI YA MASHAMBULIO

WAZIRI MKUU WA UFARANSA ATOA TAHADHALI DHIDI YA MASHAMBULIO

Like
235
0
Tuesday, 23 December 2014
Global News

 

WAZIRI MKUU wa Ufaransa Manuel Valls ametoa wito wa kuwepo uangalifu baada ya nchi hiyo kukumbwa na mashambulizi matatu ya ajabu mfululizo, na kuzusha hofu ya kutokea mashambulizi mengine kama hayo.

Katika tukio la hivi karibuni lililotokea katika mji wa magharibi wa Nantes, dereva aliliendesha gari lake na kuwagonga watu waliokuwa katika soko la Krismasi jana jioni, na kuwajeruhi kumi kabla ya kujichoma kisu mara kadhaa kabla ya kukamatwa.

Tukio hilo lilikuja siku moja baada ya shambulizi jingine sawa na hilo katika mji mwingine wa Ufaransa ambapo watu 13 walijeruhiwa.

 

 

Comments are closed.