WAZIRI MKUU WA UGIRIKI AENDELEZA ZIARA YAKE KATIKA MATAIFA YA ULAYA KUTAFUTA KUUNGWA MKONO

WAZIRI MKUU WA UGIRIKI AENDELEZA ZIARA YAKE KATIKA MATAIFA YA ULAYA KUTAFUTA KUUNGWA MKONO

Like
270
0
Tuesday, 03 February 2015
Global News

WAZIRI MKUU  mpya  wa  Ugiriki Alexis  Tsipras  anaendelea  na ziara  ya   mataifa  ya  Ulaya  tangu  aingie  madaraka  wiki  moja iliyopita, katika jitihada za  kutafuta kuungwa mkono mpango wa kutaka suala la kuiokoa nchi yake na mzigo wa madeni lijadiliwe upya.

Anakwenda  Italia  leo  kwa  mazungumzo  na  waziri  mkuu  Matteo Renzi.

Jana waziri mkuu huyo aliondoa  uwezekano  wa  kufanyakazi pamoja  na  kundi  la  pande  tatu la  wakopeshaji  wa  kimataifa.

Comments are closed.