WAZIRI WA MAMBO YA NJE LIBYA AONYA TAIFA HILO KUGEUKA SYRIA

WAZIRI WA MAMBO YA NJE LIBYA AONYA TAIFA HILO KUGEUKA SYRIA

Like
175
0
Thursday, 26 February 2015
Global News

WAZIRI wa Mambo ya Nchi za Nje wa Libya Mohammed Dayri ameonya kuwa Libya inaweza kugeuka Syria kutokana na kuzidi kupata nguvu makundi ya itikadi kali.

Amezitolea wito nchi za magharibi ziwapatie silaha wanajeshi wa Libya ili waweze kupambana na waasi.

Awamu nyingine ya mazungumzo ya kusaka ufumbuzi wa amani ilikuwa ifanyike kesho nchini Moroko, lakini yameakhirishwa baada ya bunge la Libya linalotambuliwa kimataifa kusema halitatuma wawakilishi kutokana na mashambulio ya hivi karibuni yaliyoangamiza maisha ya zaidi ya watu 40.

 

Comments are closed.