WENYEVITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI MIKOA WAKUTANA DAR LEO

WENYEVITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI MIKOA WAKUTANA DAR LEO

Like
224
0
Tuesday, 27 January 2015
Local News

WENYEVITI wa Chama cha Mapinduzi Mikoa, wamekutana Jijini Dar es salaam kwa lengo la kuunga mkono na kupongeza maelekezo ya Kamati Kuu ya Halmashari Kuu ya chama hichoTaifa iliyoyatoa January 13 huko Zanzibar, kwa Serikali katika kutekeleza maazimio ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu suala la Tegeta Escrow.

Akizungumza kwenye Mkutano huo, Mwenyekiti wa Wenyeviti hao wa Mikoa CCM, Bwana Mgana Msindai amesema kuwa wanaipongeza Serikali kwa kutekeleza maelekezo hayo ndani ya wakati na wanashauri kwamba na wengine wote waliohusika katika sakata hilo wachukuliwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kufikishwa Mahakamani.

Comments are closed.