WIZARA YA AFYA YAWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUSHIRIKIANA NA WIZARA HIYO

WIZARA YA AFYA YAWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUSHIRIKIANA NA WIZARA HIYO

Like
219
0
Wednesday, 12 November 2014
Local News

 WIZARA ya afya na Ustawi wa Jamii imewataka Waandishi wa Habari kushirikiana na Wizara hiyo katika kutoa taarifa sahihi ili kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi kutokana na taarifa zisizo sahihi.

Wito huo umetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dokta SEIF RASHID wakati akifafanua Muongozo kutoka kwa Mheshimiwa EZEKIA WENJE wa kutaka kujua Mikakati ya Serikali juu ya taarifa mbalimbali za Wizara hiyo zinazotolewa na kuandikwa katika vyombo vya Habari.

Comments are closed.