WIZARA YA MAJI IMELIOMBA BUNGE KUHIDHINISHA SHILINGI BILIONI 455

WIZARA YA MAJI IMELIOMBA BUNGE KUHIDHINISHA SHILINGI BILIONI 455

Like
225
0
Friday, 05 June 2015
Local News

WIZARA ya Maji imeliomba Bunge kuidhinisha kiasi cha shilingi bilioni 455, milioni 900 laki 9 na elfu 81 kwaajili ya kuboresha utekelezaji wa miradi ya maji katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2016.

 

Akiwasilisha makadilio ya matumizi ya wizara, waziri wa wizara hiyo Profesa JUMANNE MAGHEMBE amesema kuwa kiasi hicho cha fedha kitasaidia kurahisisha ukamilishaji wa miradi hiyo ambapo kati ya kiasi hicho shilingi bilioni 17 zitatumika kwaajili ya mishahara.

 

Kwa upande wake kamati ya kudumu ya bunge ya kilimo, mifugo na maji kupitia kwa mwenyekiti wake Profesa PETER MSOLLA imeishauri serikali kuangalia upya suala la kuweka dawa za kutibu maji katika kila eneo kwa manufaa ya Afya ya binadamu.

Comments are closed.