RAIS WA VIETNAM AANZA ZIARA YAKE NCHINI

RAIS WA VIETNAM AANZA ZIARA YAKE NCHINI

Like
328
0
Wednesday, 09 March 2016
Local News

RAIS wa Vietnam Truong Tan Sang tayari ameanza ziara yake ya siku tatu nchini ambapo leo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dokta John Pombe Magufuli Ikulu Jijini Dar es salaam.

Katika ziara yake Rais Truong Tan Sang atapata nafasi ya kuonana na Rais mstaafu wa awamu ya nne ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi-CCM-dokta Jakaya Mrisho Kikwete katika ofisi za chama hicho zilizopo Lumumba.

Lengo la ziara hiyo ni kuimarisha zaidi uhusiano uliopo kati ya nchi hizo mbili katika masuala mbalimbali muhimu ikiwemo Uchumi na Kisiasa.

PICHA 30

Comments are closed.