CANADA: ONGEZEKO LA JOTO LAUA WATU 130

CANADA: ONGEZEKO LA JOTO LAUA WATU 130

3
994
0
Wednesday, 30 June 2021
Slider

Watu zaidi ya 130 wamefariki nchini Canada kutokana na joto lisilo la kawaida kupiga ambalo limevunja rekodi ya kiwango cha joto.

Polisi wa British Columbia wamepokea taarifa za vifo tangu Jumatatu, vifo vingi vikijumuisha wazee.

Wanasema kiwango hicho cha joto kupiga katika eneo hilo kilisababisha vifo hivyo.

Jumanne, kiwango cha joto nchini Canada kiliongezeka zaidi ikawa siku ya tatu mfululizo -ilikuwa nyuzi joto 49.5 huko Lytton, British Columbia.

Kabla ya wiki hii , kiwango cha joto cha Canada hakikuwahi kuvuka nyuzi joto 45.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *