ANNIE IDIBIA: NATAMANI NINGEKUWA MAMA WA WATOTO WOTE 7 WA 2FACE

ANNIE IDIBIA: NATAMANI NINGEKUWA MAMA WA WATOTO WOTE 7 WA 2FACE

Like
392
0
Tuesday, 27 January 2015
Entertanment

Kutoka kwenye jarida la Style Magazine ambalo chapisho lake jipya nimejikita kwenye kuyajua maisha ya uzazi kwa star wa kike

Jarida hilo limetoka na stori ya muigizaji Annie Idibia kutokea Nollywood ambae pia ni mke wa mwimbaji 2face Idibia wote kutkea Nigeria

Annie Idibia ambae ni mzazi wa mabinti wawili Isabella na Olivia, ameelezea jinsi gani wazazi wake walivyoachana waliathiri mfumo wa maisha yake utotoni, ndoa yake na 2face, watoto wa kambo, ujauzito n.k

Kuhusu kutarakiana kwa wazazi wake Annie alisema

‘’ilituathiri saana kwani ilikuwa ngumu na sio kitu ambacho ningependa wanangu kiwakute kwani ukiyazoea maisha ya kuwa na wazazi wawili alafu baadae unajikuta unabaki na mzazi mmoja labda ukabaki tu na malezi ya mama na kujiuliza yuwapi baba’’

aliendelea kwa kusema mama yake alikuwa mtu shupavu kwani richa ya kuwa mama wa nyumbani tu, ilimrazimu ahusike na majukumu yote yakulea familia hivyo ilimbidi afanye kazi ilia pate kuwalea watoto wake wane na watoto pia wakijikuta wanafanya kazi ndogondogo ili kusaidia

kuhusu ndoa yake na 2face alisema

‘’nimeolewa na mchamungu na mwanaume wa pekee duniani naamini katika ndo yetu ni karibu sawa na ndoa nyingine kwani yeye ni baba mzuri na mume bora’’.

Kuhusu watoto wemgine wa 2face alisema

‘’Kwa mara ya kwanza nilikuwa nikisikia kwa watu kuhusu watoto hao na mara ya pili ni pale tulipoamua kukaa na kuzungumza na kufikia maamuzi ya kuvunja mahusiano yetu, tuligundua haikuwa na maana kuwa pamoja hivyo ni bora kuvunja mahusiano. Hiyo ilikuwa ni baada ya kuwa na Isabella’’ aliendelea kusema Annie

Kuhusu kufanya mabadiliko na kurudiana alisema

Natamani ningekuwa mama mzazi wa watoto wake wote saba ila pia ni wanangu nawapenda saana kila kilichotokea kilitokea kwa uzuri tu

Jinsi gani watoto wan je wameathiri ndoa yao

Alisema siwezi sema ni rahisi siwezi kuongopa, una watoto wa watu hivyo hamuwezi ishi kama maadau badala yake mtakuwa na mahusiano mazuri na Mungu anasimamia kwenye hili

Comments are closed.