Auawa na simba aliyemfuga nyumbani kwake

Auawa na simba aliyemfuga nyumbani kwake

Like
742
0
Wednesday, 06 March 2019
Global News

Mwanamume mmoja ameshambuliwa na simba aliyemfuga nyumbani kwake mashariki mwa Jamhuri ya Czech

Michal Prasek alimmiliki simba huyo mwenye miaka 9 na simba jike aliyemfuga kwa ajili ya kuzalisha , hatua inayoarifiwa kuzusha wasiwasi kutoka kwa wakaazi.

Babake Prasek aliupata mwili wake ndani ya kizuizi cha simba huyo na kuambia vyombo vya habari kwamba kilikuwa kimefungwa kwa ndani.

Wanyama hao waliokuwa wanaishi katika vizuizi tofuati, walipigwa risasi na kuuawa na polisi walioitwa katika eneo hilo.

Msemaji wa polisi amewaambia waandishi habari kwamba ilikuwa muhimu kwa simba hao kuuliwa ili kumfikia marehemu.

Prasek, mwenye umri wa miaka 33, alimnunua simba huyo mnamo 2016 na simba jike huyo mwaka jana, na aliwaweka wote katika vizuizi alivyovitengeneza katika ua lake katika kijiji cha Zdechov.

Awali alikatazwa ruhusa ya kujenga vizuizi hivyo, na alitozwa faini kwa kufuga wanyama hao kinyume na sheria.

Lakini mvutano wake na maafisa wa utawala ulifikia mkwamo baada ya kukataa kuruhusu mtu yoyote kuingia kwake.

Ukosefu wa vituo mbadala katika Jamhuri hiyo ya Czech, imemaanisha kwamba haingewezekana wanyama hao kuondolewa kwa lazima.

Prasek aligonga vichwa vya habari mwaka jana baada ya mwendesha baiskeli kupambana na simba hao wakati Prasek alipokuwa akiwatembeza huku akiwa amewafunga kwenye nyororo.

Baada ya polisi kuingilia kati, tukio hilo lilitazamwa kama ajali ya trafiki.

“Tukio la leo huenda likasaidia hatimaye kutatua tatizo hili la muda mrefu,” amesema meya wa Zdechov , Tomas Kocourek.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *