AZAM YASHINDWA KUTAMBA KWA URA

AZAM YASHINDWA KUTAMBA KWA URA

Like
280
0
Thursday, 18 December 2014
Slider

Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam FC jana usiku walipokea kichapo cha pili mfululizo katika ziara yao ya huko nchini Uganda. Wanalambalamba hao imechapwa goli 1-0 dhidi ya URA katika mchezo uliochezwa jijini Kampal, Uganda.

Kikosi hicho ambacho kipo chini ya kocha Mcameroon Joseph Marius Omog na Mganda, George “Best” Nsimbe imeweka kambi Uganda kujiandaa na Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyosimama kwa mwezi mmoja, ambayo itarejea wiki ijayo.

Katika dirisha dogo la usajili Azam FC imewasajili beki Serge Wawa Pascal raia wa Ivory Coast, Brian Majwega na Amri Kiemba ili kuimarisha kikosi hicho kinachoshika nafasi ya pili nyuma ya vinara Mtibwa Sugar.

Comments are closed.