RAHEEM STERLING AIPELEKA LIVERPOOL NUSU FAINALI CAPITAL ONE CUP

RAHEEM STERLING AIPELEKA LIVERPOOL NUSU FAINALI CAPITAL ONE CUP

Like
289
0
Thursday, 18 December 2014
Slider

Kiungo wa kimataifa wa England Raheem Sterling aipeleka klabu ya Liverpool katika hatua ya nusu fainali ya kombe la ligi (Capital One Cup) baada ya kufunga magoli mawili katika mchezo dhidi ya klabu ya Bournemouth.

Liverpool iliingia katika mchezo huo wa robo fainali ikiwa na jeraha la kuchapwa magoli matatu kwa sifuri dhidi ya mahasimu wao Manchester Unired, ilipata goli la kwanza mnamo dakika ya 20 kupitia kwa Sterling kabla ya Lazar Markovic kuongeza goli la pili mnamo dakika ya 27. Sterling alifunga goli la tatu mnamo dakika ya 51 huku mshambuliaji Gosling akiwafungia Bournemouth goli la kufutia machozi mnamo dakika ya 57.

rahi

Liverpool inayonolewa na kocha Brendan Rodgers inataraji kucheza na klabu ya Arsenal mwishoni mwa wiki hii huku mchezo wa nusu fainali dhidi ya Chelsea itachezwa tarehe 19 Jan 2015.

rah3

Wakati huohuo klabu ya Spurs imeibuka na ushindi wa magoli manne kwa sifuri dhidi ya Newcastle United na kutinga hatua ya nusu fainali ambapo watamenyana na Sheffield United waliitoa Southampton.

Comments are closed.