BAGHDAD: SHAMBULIZI LA KUJITOA MUHANGA LAUA WATU 15

BAGHDAD: SHAMBULIZI LA KUJITOA MUHANGA LAUA WATU 15

Like
227
0
Friday, 26 February 2016
Global News

 

KIASI cha watu 15 wameuawa kufuatia shambulizi la kujitoa muhanga linalodaiwa kufanywa na watu wawili wanaoshukiwa kuwa   na mahusiano na wanamgambo wa  kundi la itikadi kali la Dola la Kiisilamu katika eneo la msikiti wa kishia mjini Baghdad.

 

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya madaktari na polisi   watu wengine 50 wanadaiwa kujeruhiwa katika tukio hilo.

 

Duru zinaarifu kuwa mtu wa kwanza  alijitoa muhanga na kufuatiwa  na wa pili ambaye pia alijilipua baada ya maafisa usalama kufika katika eneo hilo  na kuongeza kuwa baadhi ya wahanga wa tukio hilo  ni maafisa wa vyombo vya usalama nchini humo.

Comments are closed.