ZUMA ALAANI MATUKIO YA KUCHOMA MOTO VYUO AFRIKA KUSINI

ZUMA ALAANI MATUKIO YA KUCHOMA MOTO VYUO AFRIKA KUSINI

Like
189
0
Friday, 26 February 2016
Global News

RAIS wa Afrika Kusini Jacob Zuma amelaani matukio ya kuchomwa moto kwa vyuo vikuu nchini humo.

 

Rais Zuma amesema hasira haipaswi kuwafanya baadhi ya  wanafunzi kufanya vitendo vinavyoweza kuwakosesha kupata huduma ya elimu pamoja na wenzao.

 

Kauli hiyo ya Rais Zuma inafuatia matukio ya hivi karibuni yanayodaiwa kufanywa na wanafunzi nchini humo ya  kuyachoma moto majengo ya vyuo kadhaa kwa madai ya kupinga ongezeko la ada za masomo pamoja na masuala ya ubaguzi.

Comments are closed.