BAHRAIN YAVUNJA UHUSIANO WA KIBALOZI NA IRAN

BAHRAIN YAVUNJA UHUSIANO WA KIBALOZI NA IRAN

Like
213
0
Monday, 04 January 2016
Global News

BAHRAIN imetangaza kwamba imevunja uhusiao wa kibalozi na Iran, saa chache baada ya Saudi Arabia kuchukua hatua.

 

Saudi Arabia iliwapa maafisa wa ubalozi wa Iran siku mbili kuondoka nchini Saudi Arabia kufuatia mvutano uliotokana na kuuawa kwa muhubiri maarufu wa Kishia.

 

Muhubiri huyo Sheikh Nimr al-Nimr aliuawa pamoja na watu wengine 46 baada ya kupatikana na makosa yanayohusiana na ugaidi.

Comments are closed.