LA LAKERS YAFIKIRIA KUSTAAFISHA JEZI 2 ZA KOBE BRYANT

LA LAKERS YAFIKIRIA KUSTAAFISHA JEZI 2 ZA KOBE BRYANT

Like
313
0
Monday, 04 January 2016
Slider

Timu ya mpira wa kikapu ya Los Angeles Lakers yafikiria kustaafisha jezi 2 alizovaa Kobe Bryant ndani ya kikosi hicho.

Kobe ametangza kustaafu mpira wa kikapu mwishoni mwa msimu huu 2015/16, alisajiliwa na LA Lakers mwaka 1996 na kupewa jezi namba 8 baada ya jezi mbili alizokuwa anazitaka, jezi namba 33 ilikuwa tayari imeshastaafishwa kwa heshima ya Legendary Kareem Abdul- Jabbar na ile ya namba 24 ilikuwa inavaliwa na George McCloud hivyo ilimbidi Kobe avae jezi namba 8,

Akiwa anavaa jezi namba 8 Kobe amechukuwa mataji 3 ya NBA akiwa na Lakers na baada ya kubadilisha jezi kwenda namba 24  msimu wa 2006/7 ametwaa mataji mawili.

Comments are closed.