BARCELONA MBIONI KUMUONGEZEA MKATABA NEYMAR

BARCELONA MBIONI KUMUONGEZEA MKATABA NEYMAR

Like
377
0
Tuesday, 23 December 2014
Slider

Uongozi wa klabu ya FC Barcelona upo mbioni kumuongeza mkataba wa miaka miwili nahodha wa timu ya taifa ya Brazil na mshambuliaji wa klabu hiyo Neymar utakaomalizika mwaka 2018.

Mkataba wa sasa wa Neymar unataraji kuisha mwaka 2018 ila kiwango kizuri alichokionyesha Mbrazil huyo kimewashawishi viongozi hao kutaka kumsainisha mkataba mpya ili kumzuia asijiunge na klabu nyengine.

Neymar amefanikiwa kuunda mahusiano mazuri na nahodha wa timu ya taifa ya Argentina na mshambuliaji hatari duniani Lionel Messi pamoja na Luis Suarez.

Neymar ameshafanikiwa kufunga magoli 14 na kutoa pasi 3 za magoli ndani ya michezo 18 msimu huu atakuwa nalipwa kiasi cha euro million 5 kiwango sawa na Mruguay Luis Suarez.

Comments are closed.