CHELSEA YAILAZA 2-0 STOKE CITY

CHELSEA YAILAZA 2-0 STOKE CITY

Like
370
0
Tuesday, 23 December 2014
Slider

Klabu ya soka ya Chelsea imefanikiwa kupata ushindi wa magoli mawili kwa sifuri dhidi ya Stoke City na kujihakikishia nafasi ya kwanza kuelekea katika msimu wa sikukuu ya Christmas.

Magoli ya Chelsea yamefungwa na beki na nahodha wa klabu hiyo John Terry huku kiungo wa Kihispania Cesc Fabregas akifunga goli la pili la mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Brittania.

CH2

CH

Chelsea imefikisha alama 42 ikiwa ni 5 dhidi ya klabu ya Manchester City inayoshika nafasi ya pili huku historia ikionyesha kuwa katika misimu ambayo Chelsea imekuwa ikiongoza mpaka Christmas basi huenda kulitwaa taji hilo.

Kikosi hicho cha kocha Jose Mourinho kitarejea tena uwanjani mnamo tarehe 26 mwezi huu kwa kuikaribisha mahasimu wao wa jiji la London klabu ya West Ham kabla ya kusafiri kwenda kumenyana na Southampton tarehe 28 mwezi 12 mwaka 2014.

Comments are closed.